JUHUDI ZA SERIKALI KUKABILI MPOX
Wizara ya afya imetangaza kwamba taifa linajizatiti kuweka mikakati ya kuzuia mlipiko wa ugonjwa wa Mpox na wala si kutibu, na kuhimiza ushirikiano wa dharura.
Mkurugenzi mkuu wa idara ya afya Dr. Patrick Amoth, amesema pana haja ya kuzuia ugonjwa huo mapema ili kukabili kuenea kwake, akitolea mfano wa virusi vya Korona.
Haya yanajiri baada ya ugonjwa huo kuripotiwa nchini mwezi jana ingawa mgonjwa huyo aliyekuwa safarini kuelekea Rwanda kutoka Uganda, ameripotiwa kupona.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 




















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































