#Local News

RUTO AMWOMBOLEZA MBUNGE WA ISIOLO SOUTH

Risala za rambi rambi zimeendelea kutolewa kuhusiana na kifo cha mbunge wa Isiolo South Tubi Bidu, aliyefariki hapo jana katika Nairobi Hospital alikokuwa akipokea matibabu.

Kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii X, Rais William Ruto amemtaja Bidu kama mtumishi wa umma aliyejitolea kupigania elimu, aliyeamini katika kuimarisha jamii kupitia ujuzi na fursa.

Mbunge huyo ambaye amekuwa kwenye muhula wake wa kwanza, alikuwa mwanachama wa kamati ya mazingira, misitu na madini katika bunge la kitaifa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

RUTO AMWOMBOLEZA MBUNGE WA ISIOLO SOUTH

PROF. OKOWA ACHAGULIWA JAJI ICJ

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *