MGOMO WA WAHADHIRI WANG’ATA VYUO VIKUU
Athari za mgomo wa wahadhiri zimeanza kujitokeza kwa siku ya 3 sasa, wanafunzi wakikosa kuanza masomo yao kwa muhula huu jinsi walivyokuwa wametarajia huku wahadhiri wakishikilia kuwa hawatarejea kazini hadi malalamishi yao yashughulikiwe.
Wahadhiri wanashinikiza kutekelezwa kwa makubaliano yao na serikali, kwenye mkataba wa mwaka 2021-25 waliotia Saini na serikali.
Hata hivyo, Waziri wa elimu Julius Ogamba amewahimiza kurejea kazini, akisema serikali imeanza kutekeleza makubaliano hayo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































