ODM YAPATA PAA MAGARINI
Chama cha ODM kimepigwa jeki katika uchaguzi mdogo wa Magarini kaunti ya Kilifi baada ya mwaniaji wa kiti hicho kupitia chama cha PAA Michael Kingi kujiondoa ili kumuunga mkono mwaniaji wa ODM Harrison Kombe.
Kupitia taarifa, PAA imesema kujiondoa kwa Kingi kumetokana na mashauriano na viongozi wengine waliojumuishwa kwenye serikali jumuishi.
Aidha, PAA imesema uamuzi huo unaishia kwenye uchaguzi mdogo ila kitamuunga mkono Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































