UN MBIONI KUREJESHA UTULIVU DRC
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limeandaa kikao cha pili kujadili hali tete iliyoko mashariki mwa taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.
Mkutano huo umeitishwa na viongozi wa DRC kutokana na mapigano ya kundi la waasi la M 23 ambalo limeuteka mji wa Goma na uwanja wa ndege.
Waziri wa masuala ya kigeni wa DRC Therese Kayikwamba amekosoa agizo la baraza hilo kutaka vikosi vya kigeni vya usalama kuondoka nchini humo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































