MAHAKAMA YAPINGA OMBI LA MAGAVANA KUHUSU MALIPO YA UZEENI
Magavana wamepata pigo baada ya mahakama kuu kuamuru kwamba magavana na manaibu wao hawana haki ya kupokea marupurupu ya uzeeni katika mpango sawa na ule wa maafisa wakuu katika serikali ya kitaifa.
Uamuzi huo umetolewa kufuatia kesi iliyowasilishwa na baraza la magavana dhidi ya tume ya kuratibu mishahara ya wafanyakazi wa umma SRC inayosema serikali haina uwezo wa kuwaorodhesha magavana na manaibu wao kwenye mpango huo.
Aidha, SRC inashikilia kwamba endapo ombi lao litatekelezwa, hatua hiyo itaathiri maafisa wakuu katika serikali za kaunti na ile ya kitaifa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































