WAKENYA WALAMIKA KUTOKANA NA GHARAMA YA MAFUTA
Huku Serikali ikipunguza ushuru wa VAT hadi asilimia Nane na kupunguza bei ya mafuta hapo Jana, maoni tofauti yameibuliwa kutoka sekta mbali mbali.
Wananchi wamesema kuwa mikakati iliyochukuliwa na serikali hapo jana bado haitoshi huku wakitaka serikali kuchukua hatua zaidi na kupunguza bei ya mafuta.
Aidha, wamesema kuwa hali hiyo itaathiri vikubwa maisha ya kawaida wa wakenya huku wakihofia kugharimika zaidi wakati shule zinapofunguliwa wiki ijayo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































