KOOME AONYA TUME YA ARDHI KUHUSU UADILIFU
Jaji Mkuu Martha Koome ameitaka Tume ya Kitaifa ya Ardhi kuzingatia uadilifu na uwazi katika utekelezaji wa majukumu yake.
Akizungumza wakati wa kuapishwa kwa makamishna wapya wa tume hiyo, Koome amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji ili kujenga imani ya wananchi.
Wakati huo huo, makamishna wapya wa tume ya ardhi nchini wameapishwa rasmi kuanza kuhudumu katika majukumu yao.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































