#Local News

WAKAZI WA BWAWA LA NAIROBI WATAKIWA KUHAMA

Wakazi wanaoishi maeneo ya chini ya bwawa la Nairobi kama vile Kibra, Lang’ata, South C na Madaraka wametakiwa kuhama kufuatia kupanda kwa kiwango cha maji kwenye bwawa hilo, ambayo yanahofiwa kusababisha maafa.

Kwenye tahadhari yake, mamlaka ya raslimali za maji, WRA, imesema kiwango hicho kimefikia hali ya hatari, na kuwataka wakazi kuhamia maeneo salama mapema, huku idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko nchini ikifikia watu 83 kufikia jana.

Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja, ameonya dhidi ya siasa kuingizwa kwenye tahadhari hiyo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *