ODADA AUNGA MKONO MAANDALIZI YA AFCON 2027
Kiungo wa Harambee Stars Richard Odada ameunga mkono maandalizi ya timu hiyo kuelekea mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027.
Odada amesema mazoezi ya kiwango cha juu yanayoendelea pamoja na uzoefu walioupata katika FIFA Series yatakuwa muhimu katika kuimarisha ushindani wa timu hiyo.
Kenya, ikiwa pamoja na Uganda na Tanzania, itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo, huku kocha mkuu Benni McCarthy akilenga kuiwezesha timu hiyo kufika hatua ya mtoano.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































