#Football #Sports

TUCHEL AHOJI KIKOSI BAADA YA KIPIGO

Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Thomas Tuchel, amesema sasa ana uelewa zaidi kuhusu kikosi chake licha ya kipigo cha mabao 1-0 dhidi ya Japan katika mechi ya kirafiki.

Tuchel alikuwa ameteua kikosi cha wachezaji 35 kwa mechi dhidi ya Uruguay na Japan, huku sare ya 1-1 dhidi ya Uruguay ikihusisha wachezaji wa akiba ambao hawakuvutia sana.

Kocha huyo alitarajia kuwatumia wachezaji wake wa kikosi cha kwanza, lakini mipango yake ilivurugika kutokana na kuondolewa kwa baadhi ya wachezaji, hali inayozua maswali zaidi kuelekea Kombe la Dunia.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *