#Sports

ST. ANTONY’S YALENGA UBINGWA KISUMU

Kocha wa timu ya magongo ya St. Antony’s Kitale, Kevin Lugalia, amesema kikosi chake kitachukulia kila mechi kama fainali katika michezo ya kitaifa ya shule za upili itakayoanza Jumatatu jijini Kisumu.

Lugalia amesema timu imeimarisha maandalizi yake na inaamini ina uwezo wa kutwaa ubingwa katika mashindano hayo.

St. Antony’s imepangwa katika Kundi A pamoja na Kisumu Day, Alliance High School na Mbooni Boys, kundi ambalo kocha amesema lina ushindani mkali.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *