#Local News

SERIKALI YAPUNGUZA BEI YA MAFUTA

Wakenya wamepata afueni ndogo baada ya mamlaka ya kudhibiti kawi na petroli, EPRA, kupunguza bei ya mafuta ya petroli kwa shilingi 9.37 na diseli kwa shilingi 10.21, baada ya kupunguza ushuru wa thamani ya ziada, VAT kutoka asilimia 13 hadi asilimia 8.

Kulingana na EPRA, lita moja ya petroli jijini Nairobi itauzwa kwa shilingi 197.60 na diseli 196.63 huku bei ya mafuta taa ikisalia bila mabadiliko na itaendelea kuuzwa kwa shilingi 149.49.

Tangazo la EPRA linajiri baada ya Rais William Ruto hapo jana kutangaza kupunguzwa kwa bei ya mafuta ili kuwalinda wakenya.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SERIKALI YAPUNGUZA BEI YA MAFUTA

NIKO KADI: 170 WAKAMATWA KITALE

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *