#Local News

WAFANYAKAZI WA VIWANJA VYA NDEGE KUGOMA TENA

Mamlaka ya viwanja vya ndege nchini ina muda wa siku 6 kushughulikia malalamishi ya wafanyakazi wa viwanja hivyo ambao wameonya kuwa watagoma na kutatiza shughuli katika viwanja hivyo iwapo ilani yao itapuuzwa.

Kwenye makataa ya siku 7 yaliyotolewa hapo jana, muungano wa wafanyakazi hao, KAWU, unataka mamlaka hiyo itekeleze makubaliano yaliyotiwa saini mwezi jana, mbali na kumrejesha kazini mfanyakazi aliyefutwa kazi Desemba mwaka jana jinsi mahakama ilivyoagiza.

Katibu mkuu wa KAWU Moss Ndiema, amelalamikia kufutwa kazi kwa mfanyakazi mwingine wiki jana.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAFANYAKAZI WA VIWANJA VYA NDEGE KUGOMA TENA

VYUO VIKUU VYAMEZWA NA MADENI

WAFANYAKAZI WA VIWANJA VYA NDEGE KUGOMA TENA

UTABIRI: MVUA KUONGEZEKA IJUMAA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *