SERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA BEI YA MAFUTA
Serikali imeshinikizwa kuweka mikakati mwafaka ili kuwalinda wakenya dhidi ya gharama ya juu ya maisha kwa kuhakikisha kuwa inapunguza bei ya mafuta licha ya shinikizo katika soko la kimataifa.
Katika kikao na wanahabari, mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro ambaye amekuwa mkosoaji wa serikali kuhusu mzigo wa ushuru, ameitaka serikali kuweka ruzuku mbali na kupunguza ushuru wa ongezeko la thamani, VAT.
Wito huo unajiri huku EPRA ikipunguza VAT kwa bidhaa za petroli kutoka asilimia 16 hadi asilimia 13.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































