#Local News

WANDAYI, ONE PETROLEUM WAVUTANA KUHUSU MAFUTA

Vuta nikuvute imeibuka baina ya wizara ya kawi na kampuni ya One Petroleum iliyoagiza tani 60,000 za pteroli, baada ya waziri wa kawi Opiyo Wandayi kuagiza kwamba shehena hiyo irejeshwe ilikotoka.

Hata hivyo, kampuni hiyo imepinga amri ya Wandayi, ikisema ilishinda kihalali tenda ya uagizaji mafuta, ikiwa ni miongoni mwa kampuni 4 zilizopewa tenda hiyo nje ya mfumo wa uagizaji wa kati ya serikali na serikali, G2G.

Kulingana na Wandayi, takribani shilingi bilioni 4 zingeokolewa iwapo ununuzi huo ungefanywa kupitia mfumo wa G2G.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *