#Local News

SIFUNA KUFAHAMU HATMA YAKE YA KUFURUSHWA LEO

Katibu mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna, atafahamu hatima yake hii leo kuhusiana na kutimuliwa kutoka wadhifa huo, kwenye uamuzi ambao utatolewa leo na jopo la kushughulikia mizozo ya vyama vya kisiasa nchini.

Jopo hilo awali lilitoa agizo la kuzuia kwa muda utekelezaji wa uamuzi wa baraza kuu la ODM kumfurusha Sifuna kama katibu mkuu hadi wakati ambapo kesi ya Sifuna ingesikilizwa na kuamuliwa.

Kwenye uamuzi wa leo, Sifuna atabaini iwapo ataendelea kuhudumu kama katibu mkuu wa chama hicho au safari inatamatika.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SIFUNA KUFAHAMU HATMA YAKE YA KUFURUSHWA LEO

WANGA AKANA LINDA MWANANCHI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *