DCI YAFICHUA UOZO KATIKA KABURI LA PAMOJA KERICHO
Miili yote 33 iliyofukuliwa kutoka kaburi la pamoja katika eneo la Makaburini kaunti ya Kericho, ilitolewa katika makafani ya hospitali ya rufaa na mafunzo ya kaunti ya Nyamira, tofauti za taarifa za awali kwamba makafani hiyo iliruhusu miili 13 pekee.
Kulingana na mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa jinai, DCI, Mohammed Amin, uchunguzi wa awali na tathmini ya kamera za CCTV zimethibitisha kuwa miili yote ilitoka kwenye makafani hiyo.
Miongoni mwa wanaosakwa ni wazazi wa watoto 25 ambayo miili yao ilikuwa kwenye kaburi hilo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































