#Local News

KWS YAKANUSHA UHARIBIFU WA MSITU NAIROBI

Shirika la Huduma za Wanyamapori limekanusha madai yanayosambaa mitandaoni kwamba linaharibu msitu wa nyanda za juu katika Hifadhi ya Taifa ya Nairobi.

Shirika hilo limesema madai hayo yanapotosha, likieleza kuwa kazi inayoendelea ni sehemu ya mpango halali wa kuhamisha kituo cha kulea wanyama yatima cha Nairobi.

Aidha, limesema hatua hiyo inalenga kuboresha uhifadhi wa wanyamapori, ustawi wa wanyama, huduma kwa wageni na elimu ya uhifadhi, likibainisha kuwa kituo cha sasa kilichoanzishwa mwaka 1964 hakikidhi viwango vya kisasa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *