GACHAGUA ADAI SHA IKO MAGOTINI
Wizara ya afya imekanusha taarifa kwamba bima ya SHA itasambaratika ndani ya miezi 6 ijayo kutokana na mzigo wa madeni, jinsi ilivyoibuliwa na aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua.
Kwa mujibu wa Gachagua, ni wakati kwa hospitali za umma na za kibinafsi kudai malipo yao kutoka SHA kabla ya kutoa huduma kwa wagonjwa, akisema sekta ya afya itasambaratika pakubwa bima hiyo itakaposambaratika.
Hata hivyo, Waziri wa afya Aden Duale, ameyataja madai ya Gachagua kama kuwapotosha wamiliki wa hospitali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































