RUTO AONYA MAFISADI WA MAFUTA
Rais William Ruto ameonya kuwa wahusika wa mtandao wa ulanguzi katika sekta ya mafuta na petroli watakaotumia mgogoro wa Mashariki ya Kati kujinufaisha watakabiliwa na adhabu kali.
Rais amesema serikali haitaruhusu watu wachache kutumia hali ya mgogoro huo kuwanyanyasa Wakenya kupitia vitendo vya ufisadi katika sekta ya mafuta.
Akizungumza katika eneo bunge la Kilgoris, kaunti ya Narok, Ruto amesisitiza kuwa serikali yake itachukua hatua kali kuwaondoa walanguzi na makundi yote ya kifisadi katika sekta ya petroli.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































