WAWILI WAKWAMA JENGONI WESTLANDS
Shughuli za uokoaji zinaendelea katika eneo la Westlands jijini Nairobi kuwakoa wafanyakazi wawili waliokwama baada ya sehemu ya jengo la ghorofa 22 kuporomoka usiku wa kuamkia leo.
Kwa mujibu wa shirika la msaada la Kenya Red Cross, wafanyakazi wawili waliokolewa bila majereha, na kuongeza kuwa hali ya waliokwama bado haijulikani.
Mkasa huo unajiri siku 2 baada ya watu wengine 4 kufariki kwenye mkasa sawa katika eneo la Blue Estate mtaani Shauri Moyo, jijini Nairobi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































