GACHAGUA AKOSOA UBOMOAJI GIKOMBA
Aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amelaani ubomoaji uliofanyika usiku katika soko la Gikomba, akiutaja kuwa usio na utu, wa kikatili na unaolenga kuwadhulumu wafanyabiashara wadogo.
Akizungumza na wanahabari Jumanne, Machi 31, 2026, huko Makueni, Gachagua aliishutumu serikali kwa kupanga ubomoaji huo usiku, akisema hatua hiyo ni mateso kwa wananchi wanaojitafutia riziki.
Alidai kuwa maelfu ya wafanyabiashara walipoteza bidhaa zenye thamani ya mamilioni ya shilingi katika operesheni hiyo aliyoiita ya aibu iliyotekelezwa usiku.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































