#Football #Sports

KOCHA WA MURANG’A SEAL ATAKA WAITHIRA KUITWA TIMU YA TAIFA

Kocha wa Murang’a Seal, Osborne Monday, amemshawishi kocha wa timu ya taifa, Benni McCarthy, kuzingatia kumuita mshambuliaji bora wa ligi, Joe Waithira, katika kikosi cha taifa.

Waithira, kinara wa mabao katika Ligi Kuu ya SportPesa akiwa na mabao 15, hakuorodheshwa katika kikosi kilichosafiri Rwanda kwa FIFA Series 2026, jambo lililosababisha mjadala miongoni mwa mashabiki na wanasoka.

Akizungumza baada ya Murang’a Seal kupoteza 1-0 dhidi ya Shabana FC kwenye Uwanja wa Gusii, Monday alisema: “Waithira ni mshambuliaji kamili. Anastahili kuitwa katika timu ya taifa.”

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

KOCHA WA MURANG’A SEAL ATAKA WAITHIRA KUITWA TIMU YA TAIFA

KATIBU MKUU WA CAF AJIUZULU

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *