#Football #Sports

LAPORTA ACHAGULIWA TENA KAMA RAIS WA BARCELONA

Joan Laporta amechaguliwa tena kuwa rais wa Barcelona akimshinda Victor Font kuendelea kuiongoza miamba hiyo ya Catalan hadi 2031.

Mwanachama huyo mwenye umri wa miaka 63, ambaye pia alimshinda Font katika uchaguzi wa 2021, atarejelea wadhifa wake mwezi Julai baada ya kujiuzulu wiki chache zilizopita kama sehemu ya mchakato wa uchaguzi.

Karibu asilimia 42 ya wanachama wa klabu ya Barcelona walipiga kura na kufikia kura 48480. Laporta alishinda kwa asilimia 68.18 dhidi ya asilimia 29.78 ya Font.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

LAPORTA ACHAGULIWA TENA KAMA RAIS WA BARCELONA

RUTO AWATAKA WAPINZANI WAJIANDAE

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *