#Local News

RUTO AZINDUA UJENZI WA SOKO LA IKONGE, NYAMIRA

Shughuli za kibiashara katika eneo bunge la Mugirango North kaunti ya Nyamira zinatarajiwa kuimarika katika siku zijazo kufuatia uzinduzi wa ujenzi wa soko la Ikonge huku Rais William Ruto akisema shilingi bilioni 15 zimetengewa ujenzi wa masoko ya kisasa na nyumba za bei nafuu kwenye kaunti hiyo.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa soko hilo, Rais Ruto ambaye ameandamana na naibu wake Kithire Kindiki, ameahidi ujenzi wa miradi mingine kama vile barabara, uwanja wa michezo na reli.

Rais yuko kwenye ziara ya siku 4 katika eneo la Gusii.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *