WASHTAKIWA KWENYE KESI YA MUCHAI WAHUKUMIWA KIFO
Washtakiwa wanne waliohusishwa na mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kabete George Muchai mnamo mwaka wa 2015, wamepewa hudukumu ya kifo huku wenzao wawili wakihukumiwa kifungo cha miaka 10 gerezani kila mmoja.
Hakimu mkuu Lucas Onyina, alitoa uamuzi huo hapo jana baada ya kuwapata 6 hao na hatia ya mashataka kadhaa ikiwemo wizi wa kimabavu na kumiliki silaha kinyume na sheria.
Hata hivyo, wakili wa mshtakiwa wa pili Danstan Omari, amesema atakata rufaa katika mahakama ya upeo dhidi ya uamuzi huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































