NTSA YAIMARISHA DORIA BARABARANI
Mamlaka ya usalama barabarani NTSA imetangaza kutumia kamera katika maeneo maalum katika juhudi za kuimarisha usalama barabarani msimu huu wa pasaka, huku idadi ya wasafiri ikiripotiwa kuongezeka katika nyingi ya barabara nchini.
Kwa mujibu wa taarifa, maafisa wa trafiki wataimarisha doria barabarani mbali na uwepo wa mashine za kupima kasi ya magari ili kuhakikisha nidhamu miongoni mwa madereva.
NTSA imewataka watumiaji wa barabara kuzingatia sheria za trafiki kila mara ili kuepusha maafa barabarani.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































