#Local News

METHU ASISITIZA HAJUTII ‘KUMPASHA’ RUTO

Seneta wa Nyandarua John Methu, amekariri kuwa hajutii kauli zake zilizofasiriwa kama za kumkosea heshima Rais William Ruto wiki jana katika hafla ya mazishi kaunti hiyo, akisema alikuwa akitekeleza wajibu wake kikatiba kuhakikisha Rais anatekeleza majukumu yake.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Methu amewakosoa wanaodai alimshambulia Rais kwa maneno, na kwamba hakulenga kumkosea heshima.

Amekariri kuwa anamheshimu Rais ila hamwogopi.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

METHU ASISITIZA HAJUTII ‘KUMPASHA’ RUTO

WAUGUZI KNH KUANZA MGOMO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *