UPINZANI WAMTAKA OMOLLO KUJIUZULU KISA SHAMBULIO LA OSOTSI
Viongozi wa upinzani wanamtaka katibu katika wizara ya usalama, Daktari Raymond Omollo, kujiuzulu kufuatia kushambuliwa kwa Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi katika hoteli moja jijini Kisumu.
Viongozi hao Wanasema idara ya usalama inafahamu wahuni wanaohusika na mashambulizi dhidi ya wanaopinga serikali, na hivyo wanapaswa kuwajibika kwa hali hiyo.
Kwa upande wake, Osotsi ameeleza yaliyotokea akisisitiza umuhimu wa hatua za haraka kuchukuliwa ili kuhakikisha usalama wa viongozi na wananchi kwa ujumla.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































