BARASA ASUKUMA NAFASI YA ODM KAKAMEGA
Gavana wa Kakamega Fernandes Barasa ameendeleza kampeni za chama cha ODM katika kaunti hiyo akieleza sababu za Kakamega kupewa nafasi ya juu ya uongozi ndani ya chama hicho.
Akizungumza Bukura, kaunti ndogo ya Lurambi, wakati wa ugawaji wa bidhaa za kilimo, Barasa alisema nafasi ya naibu kiongozi wa chama hicho inapaswa kutolewa kwa kiongozi kutoka Kakamega.
Alisisitiza kuwa kaunti hiyo ina uungwaji mkono mkubwa wa ODM kuliko maeneo mengine ya magharibi, hivyo kustahili kupewa nafasi hiyo ya juu ya uongozi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 


















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































