UPINZANI WADAI VURUGU ZINACHOCHEWA NA SERIKALI
Huku mjadala kuhusu makundi ya wahuni kuzua vurugu katika mikutano ya kisiasa ukishika kasi, muungano wa upinzani nchini umeibua madai kwamba wahuni hao wanafadhiliwa na serikali kuvuruga mikutano ya upinzani.
Wakiwa katika hafla tofauti, kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka na mwenzake wa DCP Rigathi Gachagua, wamehofia kuwa huenda hatua ya serikali kushindwa kuyadhibiti makundi hayo ikasababisha kuibuka kwa makundi zaidi ya wahuni kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
Wameapa kuendeleza mikutano yao na wananchi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































