#Local News

NTSA YATAKA KESI YA FAINI KUTUPILIWA MBALI

Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani, NTSA, imeiomba Mahakama Kuu kutupilia mbali kesi inayopinga utekelezaji wa mfumo wa faini za papo hapo, ikisema suala hilo limepitwa na wakati.

Katika hati ya kujibu, mkurugenzi mkuu wa NTSA, Odhiambo Kondiwa, amesema mamlaka hiyo ilisitisha rasmi mpango huo Machi 27 mwaka huu hivyo kesi hiyo haina msingi wa kuendelea kusikilizwa.

Kesi hiyo iliwasilishwa na kundi la Sheria Mtaani pamoja na wakili Shadrack Wambui waliokuwa wakipinga uhalali na utekelezaji wa mfumo huo wa faini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

NTSA YATAKA KESI YA FAINI KUTUPILIWA MBALI

UJUMBE WA RUTO KUHUSU PASAKA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *