NEKESA AAPA USHINDI KABLA YA MECHI DHIDI YA AUSTRALIA
Mshambuliaji wa Harambee Starlets, Valerie Nekesa, amesema haogopi mechi ya fainali dhidi ya Australia katika michuano ya Fifa Global Series itakayofanyika kwenye Uwanja wa Nyayo.
Nekesa amesema nafasi za viwango vya ubora duniani hazitakuwa na maana wakati timu hizo zitakapoingia uwanjani, akisisitiza kuwa kila timu itakuwa na nafasi sawa ya ushindi.
Mechi hiyo inatazamwa kuwa mtihani mkubwa kwa Harambee Starlets, huku Australia wakitajwa kuwa na nafasi kubwa ya kushinda kutokana na uzoefu na ubora wao.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































