SAKAJA AONGOZA UBOMOAJI WA UKUTA WA IKULU KUREJESHA MTO NAIROBI
Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja anaongoza mpango wa kubomoa sehemu ya ukuta wa Ikulu ya Nairobi ulioko kwenye mkondo wa mto, katika jitihada za kurejesha Mto Nairobi.
Kulingana na Sakaja, sehemu ya ukuta huo iliyojengwa kwenye ukingo wa Kirichwa River pamoja na majengo yote yaliyo kwenye mkondo wa mto yataondolewa.
Ameeleza kuwa hatua hiyo ni ishara ya uongozi thabiti, akibainisha kuwa Rais ameonyesha mfano kwa kukubali kufuata kanuni za mazingira.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































