#Local News

NATEMBEYA AONYA MADAKTARI WA UMMA WANAOPUUZA WAGONJWA

Gavana wa Kaunti ya Trans Nzoia George Natembeya amesema serikali yake haitavumilia madaktari walioajiriwa na umma wanaoshindwa kuwahudumia wagonjwa ipasavyo.

Natembeya ameeleza kuwa baadhi ya madaktari wanatumia muda mwingi kuendesha kliniki zao binafsi badala ya kutekeleza majukumu yao katika hospitali za serikali, hali inayodhoofisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Ameonya kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika, akisisitiza kuwa kipaumbele cha serikali ya kaunti ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya katika vituo vya umma.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *