#Local News

HOSPITALI YA NAIROBI YAJITETEA KUHUSU HALI YA KIFEDHA

Hospitali ya Nairobi imetetea hali yake ya kifedha na uendeshaji wake ikisema huduma zinaendelea bila kukatizwa, huku ikilaumu mgogoro wa muda mrefu wa uongozi kwa taharuki iliyoshuhudiwa mahakamani na hadharani.

Katika mkutano na wanahabarimwenyekiti wa bodi Barcley Onyambu pamoja na Afisa Mkuu Mtendaji Felix Osano wamesema hospitali hiyo iko imara na inaendelea kutoa huduma kikamilifu bila kuathiri wagonjwa.

Maafisa wa hospitali hiyo pia wamepuuza takwimu zinazozunguka hadharani wakisema ni za kupotosha, wakikanusha madai ya kuwepo kwa upotevu wa shilingi bilioni 9.1, hasara ya bilioni 3 au mkopo wa bilioni 4.2 unaodaiwa kuchukuliwa na hospitali hiyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *