TUSKER YAJITOA MBIO ZA UBINGWA WA LIGI
Kocha mkuu wa Tusker FC, Julien Mette, amekiri kuwa mbio za ubingwa wa Ligi Kuu hazipo tena mikononi mwao, akiwataka wachezaji kuhamisha nguvu zao kwenye mashindano ya Kombe la FKF.
Timu hiyo, iliyotwaa ubingwa mara 13, itakabiliana na Kariobangi Sharks katika hatua ya 16 bora, huku ikiwa nafasi ya saba kwenye jedwali la ligi ikiwa na alama 37, nyuma ya vinara Gor Mahia kwa alama 19.
Mette amesema ni muhimu kukubali hali halisi na kuelekeza juhudi katika mashindano yanayoweza kuwaletea taji msimu huu.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































