HUZUNI YATANDA KANDUYI BAADA YA MHUDUMU WA HOTELI KUUAWA
Hali ya huzuni imetanda katika soko la Tuuti Kibabii katika eneobunge la Kanduyi, baada ya mhudumu mmoja wa hoteli kupatikana akiwa ameuawa.
Kulingana na mmiliki wa hoteli hiyo, Yusufu Majaliwa, mfanyakazi wake alionekana kupitia kamera za usalama akianguka chini, jambo linalozua shaka kuwa alivamiwa usiku.
Wakazi na wafanyabiashara wa eneo hilo wamelalamikia kudorora kwa usalama, wakisema matukio ya uvamizi yamekuwa yakijirudia na sasa wanaiomba serikali kuingilia kati na kuimarisha ulinzi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































