ZICO AREJEA POSTA RANGERS
Kocha mkongwe Zedekiah Otieno ametambulishwa rasmi kama kocha mkuu wa Posta Rangers katika uwanja wa Chuo cha Ualimu cha Thogoto.
Otieno, anayejulikana kama “Zico,” amejiunga na timu hiyo katika kipindi ambacho imekuwa ikipambana na ukosefu wa uthabiti licha ya kuanza vyema msimu.
Kwa uzoefu wa zaidi ya miaka ishirini, akiwa amewahi kuzifundisha timu kadhaa ikiwemo Gor Mahia na KCB, Zico anatarajiwa kuisaidia Posta Rangers kuboresha matokeo yake katika ligi kuu msimu unapoelekea kutamatika.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































