#Local News

MUDAVADI: HAKUNA FIDIA KWA WAATHIRIWA WA URUSI

Wakenya waliouawa au kujeruhiwa katika vita kati ya Urusi na Ukraine hawatapewa fidia na serikali, na badala yake serikali itawasaidia wanaotaka kurejea nchini kufanya hivyo.

Akizungumza jijini Moscow, Urusi, Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi, amepuzilia mbali uwezekano wa serikali kuwapa fidia wakenya hao, akisisitiza msimamo wa Urusi kwamba walijitolea kupigana katika vita hivyo.

Familia za wakenya 10 waliouawa na mamia ya waliojeruhiwa zimekuwa zikiishinikiza serikali kuwajibika.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *