MBADI: BEI YA MAFUTA IMEPANDA KIMATAIFA
Waziri wa Hazina ya Taifa, John Mbadi, amesema serikali itaingilia kati kuwalinda Wakenya dhidi ya kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli katika soko la kimataifa.
Mbadi amesema serikali itatumia fedha kutoka kodi ya maendeleo ya mafuta, inayokadiriwa kuwa shilingi bilioni 17, katika kipindi cha miezi mitatu ijayo ili kupunguza shinikizo la bei kwa watumiaji.
Ameongeza kuwa serikali pia inazingatia marekebisho ya ushuru wa thamani (VAT) kwenye mafuta, licha ya kuwepo kwa akiba ya kutosha ya mafuta nchini.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































