#Local News

VIFO VYA MAFURIKO VYAFIKIA 88

Idadi ya vifo vinavyotokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa nchini imefikia watu 88.

Kwa mujibu wa taarifa ya Huduma ya Polisi ambayo imetolewa hii leo, maelfu ya familia pia wameathiriwa huku miundombinu muhimu ikiharibiwa vibaya katika maeneo mbalimbali.

Zaidi ya familia 2,690 zimelazimika kuyahama makazi yao na kwa sasa zinaishi katika vituo vya muda huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha katika sehemu kadhaa za nchi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *