#Football #Sports

BAJABER AREJEA KIKOSI CHA TAIFA

Mchezaji wa Simba, Mohammed Bajaber, ameahidi kurejesha imani aliyopewa baada ya kuitwa tena katika kikosi cha taifa cha Harambee Stars kufuatia kipindi kigumu alichopitia kutokana na majeraha.

Kiungo huyo mshambuliaji mwenye umri wa miaka ishirini na mitatu amerejea kikosini kwa mara ya kwanza baada ya takriban mwaka mmoja, akisema kuwa kipindi hicho kilimjaribu sana kimwili na kiakili.

Bajaber amekiri kuwa mwaka uliopita ulikuwa miongoni mwa vipindi vigumu zaidi katika taaluma yake ya soka, lakini sasa ana azma ya kurejea kwa nguvu na kuonyesha uwezo wake uwanjani.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *