#Local News

KWS YAKANA KUHUSIKA NA KUTOWEKA KWA MVUVI

Shirika la kutoa hifadhi kwa wanyamapori nchini, KWS, limeendelea kujitenga na madai ya kuhusika katika kutoweka kwa mvuvi Brian Odhiambo katika mbuga ya Lake Nakuru mwanzoni mwa mwaka jana.

Akiwa mbele ya kamati ya seneti kuhusu usalama, mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Erastus Kanga, ameiambia kamati hiyo kwamba Odhiambo, anayedaiwa kukamatwa na maafisa wa KWS, hayuko kwenye rekodi za shirika hilo.

Walalamishi sasa wanataka uvuvi kwenye mbuga hiyo kuhalalishwa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *