#Local News

MARAGA AIKOSOA SERIKALI KUHUSU GHARAMA YA MAFUTA

Aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga ameikosoa serikali kwa kushindwa kuchukua hatua madhubuti za kuwalinda Wakenya dhidi ya ongezeko la gharama ya mafuta.

Akizungumza katika kaunti ya Nandi, Maraga amesema kupanda kwa bei ya mafuta kumesababisha gharama ya maisha kuongezeka kwa kiwango kikubwa, hali inayowafanya wananchi wengi kuishi kwa shida.

Ameongeza kuwa licha ya changamoto hizo, serikali inaendelea kutenga fedha nyingi kwa Ofisi ya Rais badala ya kuangazia mahitaji ya msingi ya wananchi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *