#Local News

OYUU APUUZA AZMA YA SOSSION KNUT

Katibu Mkuu wa KNUT Collins Oyuu amepuuzilia mbali azma ya mtangulizi wake Wilson Sossion ya kugombea katika uchaguzi ujao wa kitaifa wa chama hicho.

Oyuu amesema kuwa Sossion kwa sasa si mwanachama wa chama hicho, hivyo hana sifa za kushiriki katika uchaguzi wa ndani wa KNUT.

Kauli hiyo inaibuka huku kukiwa na mjadala kuhusu uongozi wa chama hicho, huku viongozi wakisisitiza umuhimu wa kufuata katiba na kanuni za chama katika uchaguzi wake.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *