#Football #Sports

OSAMA AHAMIA KLABU YA SWEDEN

Winga chipukizi wa Kenya, Paul Osama, amepiga hatua kubwa katika taaluma yake ya soka baada ya kujiunga na klabu ya Enköpings nchini Sweden akitokea Murang’a Seal.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na Murang’a Seal mwanzoni mwa msimu wa 2025/2026 akitokea Mombasa United na kujidhihirisha haraka kama mchezaji muhimu, akifunga mabao matatu muhimu.

Osama ametia saini mkataba wa miaka miwili na anatarajiwa kusafiri kuelekea Sweden wiki ijayo, huku akitarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza Aprili 4 timu yake itakapoanza msimu dhidi ya Stocksund.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *