MWANAUME AKAMATWA KWA KUMUUA BINAMU YAKE MIGORI
Polisi wamemkamata mwanamume wa miaka 27 kwa madai ya kumchoma kisu na kumuua binamu yake wa miaka 21 katika Kaunti ya Migori.
Kulingana na Naibu Chifu William Jabed, ugomvi kati ya wawili hao umesababisha mshukiwa, Fred Ngere, kurejea nyumbani kuchukua kisu kabla ya kumshambulia Charles Otieno, aliyefariki alipofikishwa hospitalini.
Mwili wake umehamishiwa Hospitali ya Migori Level Four kwa uchunguzi wa maiti.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































