#Local News

MUKHISA AAGIZWA NA CUE KUHUSU MADAI DHIDI CHUO

Tume inayosimamia elimu ya vyuo vikuu, CUE, imemwagiza aliyekuwa katibu mkuu wa idara ya biashara na ustawi chini ya Umoja wa Mataifa, Mukhisa Kituyi, kufika mbele yake kuhusiana na kauli alizotoa kuhusu chuo kikuu cha Masinde Muliro.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, CUE imesema Mukhisa, akiwa kwenye mahojiano na kituo cha redio tarehe 31 mwezi jana, alidai kwamba kuna watu waliopewa nafasi na chuo hicho kufuzu ila hakuwa wanafunzi wa chuoni humo.

Tume hiyo imemtaka ajiwasilishe na ushahidi kuhusu madai yake.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *